Psalms 46:1-5

Mungu Yuko Pamoja Nasi

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Wana Wa Kora. Mtindo Wa Alamothi)


1 aMungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu,
msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.

2 bKwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa
nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.

3 cHata kama maji yake yatanguruma na kuumuka,
milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.


4 dKuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu,
mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.

5 eMungu yuko katikati yake, hautaanguka,
Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
Copyright information for SwhKC